MAKALA 006S: Masharti katika Hati ya Umiliki
READ THIS ARTICLE IN ENGLISH
UTANGULIZI
Baada ya kufanikiwa kupata Hati ya Umiliki inashauriwa kuisoma na
kuielewa vizuri.
Miongoni mwa vitu vinavyopatikana katika Hati ya Umiliki ni masharti ya
Hakimiliki ya ardhi.
Katika Makala hii mjadala utakuwa kuhusu masharti yanayopatikana katika
Hati ya Umiliki ambayo mmiliki wa ardhi anatakiwa kuyafuata ama kuyatimiza.
Masharti hayo yanaelezwa hapa chini;
i) Kulipa Kodi ya Ardhi
Mmilki anatakiwa
kulipa Kodi ya Ardhi kila mwaka katika kipindi chote cha umiliki. Kodi ya
Ardhi inaweza kubadilishwa na Kamishna
wa Ardhi katika vipindi tofauti.
Kwa nini
tunalipa Kodi ya Ardhi?
Ni kwa namna
gani mmiliki anaweza kufahamu kiasi cha Kodi ya Ardhi anachotakiwa kulipa
katika mwaka husika?
Ni kwa namna
gani mmiliki anaweza kulipia Kodi yake ya Ardhi?
Hapa tumechochea
tu uelewa wa mwanzo kuhusu Kodi ya Ardhi
Tutakuwa na
mjadala wa kina kuhusu Kodi ya Ardhi katika moja ya makala za wiki zijazo.
ii) Kulinda Mawe ya Mipaka
Mmiliki wa ardhi
anapaswa kulinda mawe yote ya mipaka yaliyopo katika ardhi yake katika kipindi
chote cha Hakimilki.
Mawe ya mipaka
huwekwa kipindi cha upimaji wa ardhi na husaidia kutenganisha ardhi
zinazopakana.
Ikitokea mawe ya
mipaka yanakosekana katika ardhi, mmiliki anatakiwa kuyarejesha au kuweka tena
mawe hayo kwa kutumia gharama zake.
iii) Kutunza Mazingira
Mmiliki
anatakiwa kulinda na kutunza mazingira. Hii inajumuisha kulinda ardhi yake
dhidi ya mmomonyoko wa udongo.
iv) Masharti ya Ujenzi
Masharti ya
ujenzi yaliyomo ndani ya Hati ya Umiliki ni haya yafuatayo;
a) Jengo liwe katika vifaa vya
kudumu vya ujenzi.
b) Kuwasilisha ramani ya jengo
katika mamlaka husika ndani ya miezi sita (6) baada ya kuanza kwa muda wa Hati
Miliki.
c) Ujenzi wa (ma)jengo uanze ndani
ya miezi sita (6) baada ya kuthibitishwa kwa ramani ya jengo.
d) Ujenzi ukamilike ndani ya miezi
thelathini na sita (36) toka kuanza kwa muda wa Hati Miliki.
e) Sharti la nini kiwepo juu ya
ardhi. Kwa mfano, nyumba moja tu na mabanda ya kawaida na muhimu.
v) Matumizi ya Ardhi
Hati ya Umiliki
hutoa masharti ya matumizi ya ardhi husika. Mmiliki anatakiwa afuate maelekezo
yaliyooneshwa katika Hati kuhusu matumizi ya ardhi yake. Kutofuata maelekezo
hayo kunaweza kupelekea kuchukuliwa hatua za kisheria kama vile amri ya
kusimamisha ujenzi au kubomoa jengo.
Ikiwa mmiliki
anahitaji kubadilisha matumizi ya Hakimilki yake, anatakiwa kufuata taratibu
zilizowekwa za kubadilisha matumizi.
vi) Uthibitisho wa Kutoa Haki ya Umiliki kwa Kamishna wa Ardhi
Mmiliki
haruhusiwi kutoa Haki yake ya Umiliki kwa mtu mwingine ndani ya miaka mitatu
baada ya kuanza kwa muda wa Hati Miliki bila ya ithibati ya Kamishna wa Ardhi
vii) Kutoa Taarifa ya Miamala ya Ardhi kwa Kamishna wa Ardhi
Ni lazima
taarifa iwe katika fomu maalumu na itolewe kabla au wakati muamala unafanyika.
Pia iambatanishwe na tozo na kodi zinazohusiana na muamala huo.
viii) Kufuta Hati ya Umiliki
Nchini Tanzania, mamlaka ya mwisho ya umiliki wa ardhi yamekabidhiwa kwa
Raisi (Hati ya Hatima). Hivyo, Rais anaweza kufuta Hati ya Umiliki kwa nia
njema au manufaa ya umma.
Unataka kujifunza zaidi?
Tazama video hii inayoelezea masharti ya umiliki wa ardhi.
Unataka kujifunza zaidi?
Tazama video hii inayoelezea masharti ya umiliki wa ardhi.
Ahsante na karibu sana!
The Aliland Team
Comments