Maana ya Ardhi na Mgawanyo wa Ardhi Nchini Tanzania
SEHEMU A
Maana ya Ardhi
Kuna tafsiri kadhaa za ardhi ambazo zimetolewa na makundi mbalimbali kama vile dini, wanajiografia na wanauchumi.
Hata hivyo, inafaa zaidi kutumia tafsiri iliyotolewa na
Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 ambayo inatafsiri kuwa;
"Ardhi" ni ile inayojumuisha vitu vyote vilivyo juu na chini ya uso wa nchi vikiwemo majengo, uoto wa asili na maendelezo yote yaliyofanywa isipokuwa madini na bidhaa za mafuta na gesi"Pengine utakuwa umegundua kuwa moja ya sifa ya msingi ya tafsiri ya hapo juu ni kutojumuishwa kwa madini na bidhaa za mafuta na gesi katika ardhi.
Kwa nini petroli na aina zote za madini zinazopatikana chini ya ardhi sio sehemu ya ardhi?
READ THIS ARTICLE IN ENGLISH
SEHEMU B
Makundi ya Ardhi Nchini Tanzania
Kulingana na Kifungu 4(4)
cha Sheria Na.4 ya Ardhi, ardhi ya Tanzania imegawanywa katika makundi
yafuatayo;
a) Ardhi ya Hifadhi
b) Ardhi ya Kijiji
c) Ardhi ya Jumla
Ni Nini Lengo la Mgawanyo Huu?
a) Ardhi ya Hifadhi
b) Ardhi ya Kijiji
c) Ardhi ya Jumla
Ni Nini Lengo la Mgawanyo Huu?
Lengo ni kuwezesha
usimamizi wa ardhi chini ya Sheria Na.4 ya Ardhi ya mwaka 1999 na sheria zote
zinazohusiana na ardhi.
Makundi ya ardhi
yanaelezewa hapa chini;
a) Ardhi ya Hifadhi
Ardhi ya Hifadhi ni ardhi
inayolindwa kisheria, au ardhi iliyotengwa au kuhifadhiwa kwa matumizi maalumu
ya kitaifa au kijamii kwa manufaa ya raia au wanajamii wote.
Ardhi hii hujumuisha; hifadhi za taifa; ardhi ilihifadhiwa kwa huduma za umma; hifadhi za misitu; hifadhi za maji; hifadhi za barabara; hifadhi za maeneo ya wazi; hifadhi za wanyamapori; na ardhi ambazo kama zikifanyiwa maendelezo zitaleta hatari kwa mazingira, kwa mfano, kingo za mto. Ardhi ya Hifadhi ni asilimia 28 ya ardhi yote nchini Tanzania.
Ardhi hii hujumuisha; hifadhi za taifa; ardhi ilihifadhiwa kwa huduma za umma; hifadhi za misitu; hifadhi za maji; hifadhi za barabara; hifadhi za maeneo ya wazi; hifadhi za wanyamapori; na ardhi ambazo kama zikifanyiwa maendelezo zitaleta hatari kwa mazingira, kwa mfano, kingo za mto. Ardhi ya Hifadhi ni asilimia 28 ya ardhi yote nchini Tanzania.
Kundi hili liko chini ya
usimamizi wa sheria na mamlaka mbalimbali kutegemeana na aina ya hifadhi. Mfano, ardhi ya hifadhi za mbuga za wanyama iko chini
ya usimamizi wa Sheria ya Mbuga za Wanyama ya mwaka 2009 na chombo chenye mamlaka ya kusimamia mbuga
za wanyama ni Shirika la Hifadhi za Taifa la Wanyama (TANAPA).
b) Ardhi ya Kijiji
Hii ni ardhi iliyo ndani
ya kijiji kilichosajiliwa na kubainishwa mipaka, na ile iliyokubalika na
Halmashauri ya Kijiji husika kuwa ni ardhi ya kijiji; na ardhi ambayo si ya
hifadhi, na kwa muda wa miaka kumi na miwili au zaidi kabla ya Sheria ya Ardhi
ya Kijiji Na.5 kutungwa, wanakijiji wamekuwa wanaikalia na kuitumia kama ardhi
ya kijiji na pasipo kuwepo na aina yoyote ya umiliki au matumizi kabla au
wakati kipindi hicho. Ardhi ya kijiji
inachukua asilimia 70 ya ardhi yote nchini Tanzania.
Kundi hili la ardhi lipo chini ya usimamizi wa
Halmashauri ya Kijiji, Kamati ya Maamuzi ya Kijiji, Mkutano Mkuu wa Kijiji,
Halmashauri ya Wilaya, na Kamishina wa Ardhi.
c) Ardhi ya Jumla
Sheria ya Ardhi
inatafsiri Ardhi ya Jumla kuwa ni ardhi yote ya umma inayobaki baada ya kuondoa ardhi ya kijiji na ardhi ya
hifadhi, na inajumuisha ardhi ya kijiji ambayo haikaliwi wala
kutumiwa na wanaKijiji. Hivyo,
Ardhi ya Jumla hujumuisha mapori, ardhi ya miji, majiji na halmashauri, ambayo
hayajatengwa kwa matumizi ya umma.
Ardhi ya Jumla, kulingana na Sheria ya Ardhi ya Kijiji, ni
ardhi yote ya umma inayobaki baada
ya kuondoa ardhi ya kijiji na ardhi ya hifadhi. Tafsiri hii
haijumuishi ardhi ya kijiji ambayo haikaliwi wala kutumiwa na wanaKijiji.
Hivyo, kuna mkanganyiko wa Sheria ya Ardhi na Sheria ya Ardhi ya Kijiji katika
kutafsiri Ardhi ya Jumla.
Ardhi ya Jumla ipo chini ya usimamizi wa Kamishna wa
Ardhi.
Hitimisho
Ardhi ya Jumla na Ardhi ya Hifadhi zinasimamiwa na Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999, ilhali Ardhi ya Kijiji inasimamiwa na Sheria ya Ardhi ya Kijiji Na. 5 ya mwaka 1999.Kuna hitaji la kusawazisha tafsiri ya “Ardhi ya Jumla” katika Sheria ya Ardhi na Sheria ya Ardhi ya Kijiji ili kuondoa mkanganyiko uliopo.
Inawezekana kuhawilisha aina moja ya Ardhi kwenda kwenye aina nyingine. Uwezekano huu upo wa namna mbili kisheria;
i) Uhawilishaji wa Ardhi ya Kijiji kuwa Ardhi ya kawaida au Ardhi ya Hifadhi
ii) Uhawilishaji wa Ardhi ya kawaida au Ardhi ya Hifadhi kuwa Ardhi ya Kijiji.
Ahsante na Karibu Sana!
The Aliland Team
Comments